Amini Mitume Wake

Sura ya Biblia ya kila siku

Majadiliano

Wakati wa Kusoma: Less than one minute Sikiliza Mtandaoni Right arrow icon

1 Bwana ametamalaki, mataifa wanatetemeka; Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika. 
Bwana katika Sayuni ni mkuu, Naye ametukuka juu ya mataifa yote. 
Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa; Ndiye mtakatifu. 
Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu; Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili; Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.
Mtukuzeni Bwana, Mungu wetu; Sujuduni penye kiti cha miguu yake; Ndiye mtakatifu. 
Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake, Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake, Walipomwita Bwana aliwaitikia; 
Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao. Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa. 
Ee Bwana, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu; Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe Ingawa uliwapatiliza matendo yao. 
Mtukuzeni Bwana, Mungu wetu; Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu; Maana Bwana, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

See Previous Reading See Next Reading

JIUNGE NA MJADALA