Zaburi 121
Soma sura Jiunge na Majadiliano
Ufafanuzi
Jidhanie kama mhujaji ukieleka Yerusalemu kusherekea mojawapo ya zile siku kuu tatu. Kwa mbali unaona mlima mtakatifu, mahali ambapo Hekalu linasimama na utukufu wake unaonekana. Wewe kama msafiri mchovu macho yako kutazama hekalu, inawakilisha kuweka tumaini lako kwa Yule Mungu mwenye uwezo wote ambaye anakuwezesha kuendelea mbele hata kama njia ikiwa ngumu na machungu ya namna gani..
Kwa msafiri wa wakati ule wa Biblia, safari yake ilikuwa ngumu na wakati mwingine ya hatari kwa unyanganyi na mambo mengine. Kuweka macho yako kwa Bwana, ukimtumaini na kuelewa Ulinzi wake ni wa muhimu sana kwa wasafiri hawa na sisi pia. Joto pia nalo lilikuwa kali wakati wa mchana na wakati wa usiku utisho wa aina mbaki mbali waweza kuleta moyo kuchoka Siku zile watu waliamini mwanga wa mwezi una madhara na hata kuweza kuvurugikiwa na kichwa ‘Lunatic’. Ni faraja iliyoje Mpendwa msafiri wa mbinguni leo hili fungu linaleta kwetu leo tusafiripo kuelekea mbinguni “5 Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.
Cindy Nash
Mke, Mama, Nesi
Collegedale, Tennessee, Marekani